Laws and regulations, politics and democracy in general

Vertical Sample

Monday, November 7, 2016

SAMWEL SITA AFARIKI DUNIA, KURUNZI SA SIASA BLOG, POSTED BY ELIAS MAGUGUDI









Spika wa Bunge Mstaafu, Samuel Sitta (74) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo wakati akipatiwa matibabu nchini Ujerumani.Mtoto wa marehemu, Benjamin Sitta amesema baba yake amefariki saa 10:00 usiku wa kuamkia leo.‘’Nikweli mzee amefariki nchini Ujerumani akiwa anapatiwa matibabu, alipelekwa Alhamisi iliyopita na alikuwa anasumbulia na saratani ya tezi dume ambayo ilisambaa na kuathiri miguu na mwili mzima."Benjamin amesema kuwa taarifa za mipango ya kusafirisha mwili zitatolewa baadaye.Sitta alikuwa Spika wa Bunge tangu mwaka 2005 hadi mwaka 2010 na pia mbunge wa Urambo Mashariki.Pia, alikuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba na aliwahi kuwa waziri katika wizara mbalimbali kwa vipindi tofauti.Alikuwa miongoni mwa wanachama zaidi ya 42 wa CCM waliochukua fomu za kugombea urais mwaka jana.

Posted by Elias Magugudi
Kurunzi za Siasa
eliasmagugudi2016@gmail.com

0 comments:

Post a Comment